Wednesday, September 5, 2012

KITU KIZITO CHAUA MTU MMOJA BUTIAMA






Kamanda wa polisi  wa mkoa wa mara Absalom mwakyoma  akitoa taarifa ya kifo mbele ya waandishi wa habari.

Mtu mmoja mkazi wa kijiji cha ketasakwa wilayani butiama amefariki dunia  akikimbizwa  katika kituo cha afya  kiagata  kufuatia kupigwa na kitu kizito kichwani .

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi wa mkoa wa mara Absalom Mwakyoma alisema kuwa  mnamo 29 agosti 2012 majira  ya saa moja usiku  katika kijiji cha ketasakwa ,kata ya bwiregi ,tarafa ya kiagata  wilayani butiama mkoani mara, amemtaja marehemu  maswe 26 alijeruhiwa  kwa kupigwa  na kitu kizito kichwani  na Shera wasaga ,ambapo ugomvi huo ulitokea  katika klabu cha pombe za kienyeji.

Baada ya kupigwa kitu kizito kichwani  juhudi zilifanyika za kupelekwa  katika kituo cha afya  kiagata  kwa matibabu  lakini alifariki dunia .

Mwakyoma alisema kuwa mtuhumiwa  alitoroka  baada ya tukio hilo na jitihada za kumtafuta  na hatimaye kumfikisha  mahakamani  zinaendelea.
Mwili wa marehemu   umefanyiwa  uchunguzi  na daktari na kukabidhiwa  kwa ndugu wa marehemu  kwa mazishi.
Kamanda ametoa wito kwa wananchi  kuacha kujichukulia  sheria mkononi  kuepukana na ulevi wa kupindukia.

No comments:

Post a Comment