Friday, September 28, 2012

STR8MUZIK FREESTYLE ILIVYOBAMBA

1.Dancers
Mmoja wa wanakundi cha waburudishaji cha BFB cha mkoani Mwanza akifanya vitu vyake katika mpambano wa kusaka ma-MCs na DJs wa STR8MUZIK Freestyle 2012 mkoani mwanza uliofanyika katika ukumbi wa Stone mjini humo jana usiku.(Picha ya Excutive Solutions)
2.Kabebwa JUU
Mashabiki wa ST8MUZIK Freestyle 2012 mkoani Mwanza wakiwa wamembeba juu MC bora wa mwaka mkoani humo Joash Magadula katika mpambano uliofanyika jana usiku katika ukumbi wa Stone mjini humo.(Picha ya Executive Solutions)
3. DJ Winner
Mshindi wa mpambano wa ma-DJ wa ST8MUZIK Freestyle 2012 mkoani mwanza DJ Juma Ramadhani(Kati) akitumbuiza mara baada ya kukabidhiwa chombo cha kupigishia muziki chenye thmani ya Sh mil 7 na Meneja wa TCC Mkoa wa Mwanza Deogratius Kamugisha(Kulia), huku mshindi wa upande wa ma-MC mkoani humo Joash Magadula akishuhudia na zawadi yake mkononi.(Picha ya Executive Solutions)
4.MC Winner
Meneja wa TCC Mkoani Mwanza Deogratius Kamugisha akimkabishi tuzo MC bora wa ST8MUZIK Freestyle 2012 mkoani Mwanza Joash Magadula katika mpambano uliofanyika katika ukumbi wa Stone mjini humo jana.(Picha ya Executive Solutions)
5.Mashabiki 1,2
Umati wa wana-Mwanza ulivyoshona katika ukumbi Club Stone mjini humo katika mpambano wa STR8MUZIK 2012 FreeStyle Mwanza.(Picha ya Executive Solutions)
6.Easy Business
Msanii wa kizazi kipya Easy Business ambaye ni maarufu kwa kibao chake cha “Ongea na Mshua” akitumbuiza katika mpabano wa STR8MUZIK 2012 FreeStyle Mwanza
7.Washindi Wote
Meneja wa TCC tawi la Mwanza, Bw Deogratius Kamugisha (Katikati) akipozi na washindi wa mpambano wa ma MCs na DJs STR8MUZIK Freetyle 2012 mkoani mwanza. Kutoka kushoto ni Mshindi wa pili wa DJs Ruyobya Johannes a.k.a DJ Yt,Mshindi wa kwanza kwa DJs Juma Ramadhani,Msindi wa Pili katika kategori ya ma-MCs Nchana Antony na Mshindi wa MCs Joash Magadula a.k.a MC Magadash.(Picha ya Executive Solutions)








Picha na bin zubeiry

KOCHA MPYA WA YANGA

Kocha huyo anatokea uholanzi uku akiwa ni kocha aliyekuwa na timu ya APR katika kagame cup mwaka 2012.

BHAAAAAS!!! RICK ROSS NDANI

Msanii nguli wa marekani kutua bongo katika jukwaa kubwa la muonekano wa chupa ya serengeti.

Tuesday, September 25, 2012

STUDIO NI CHACHE LAKINI MA PRODUCER KIBAO

kushoto ni ommy runner,dj tmba,mow na mdau.

usiku mnene

MOW MATHEMATIC INDE HOUSE

Mow akifanya bonge la show ndani ya club house musoma.

DE CLUB HOUSE MUSOMA


MOW MATHEMATIC KATIKA JUKWAA LA FIESTA

Mow nikati ya wasanii wa hip hop wanao fanya vizuri hapa musoma alitoka na no dream no life mwaka jana mpaka sasa anatalajia kuachia video yake mpya siku chache zijazo nilimuuliza siku moja wewe ni g au sharo akacheka saaana!!!!!! Producer anaye fanya nae kazi hivi sasa ni Ommy Runner.

Monday, September 24, 2012

SIMBA YAZIDI KUCHANJA MBUGA KATIKA LIGI KUU

Shomari kapombe na haule kipawa ruvu shooting uso kwauso jana ligi kuu vodacom bara.
Felix sunzu aanza kazi simba baada ya kupachika bao lake la kwanza katika ligi kuu vodacom bara jana
Mrisho khalfan ngassa azidi kuchanua msimbazi.
Ronardo de lima anavyoonekana sasa hivi kiasi cha kuwafanya dr wake kujalibu kupunguza mafuta mwilini baada ya kuweka madaluga juu.

Wednesday, September 19, 2012

PPAMBANO VIDEOS PRODUCTION AKIPIGA KAZI YA VIDEO YA I DDI COM NI TRACK YATEMPTED TO TOUCHO IM

Iddi com akiwa anafanya shooting na walembo kazi ilichukua siku kadhaa mpaka kukamilika kaamkao wa kula utaipata kupitia vituo mbali mbali vya TV na Radio za bongo na Afrika mashariki

I DDI COM ATOKELEZEA NA SINGLE MPYA

Siku ya fiesta alitambulisha single yake katika jukwaa kubwa la muonekano mpya wa serengeti bia track inayo kwenda kwa jina la TEMPTED TO TOUCH katika uwanja wa Karume musoma mjini

Abdalah nyaganya aka chikaka!!!!!!! msanii anayetamba na single yake kanda ya ziwa !!

Mmoja kati ya wasanii wanaokuja juu kwa muziki wa kizazi kipya katika kanda ya ziwa maeneo ya musoma mjini na viunga vyake ni chikaka jamaa natamba na nyimba mbili ametoa single ya kwanza inayoitwa itwa (Utanaswalo) ni kijita lugha ya watu wa musoma majita akimaanisha Hauna aibu! track hiyo amemshilikisha msanii wa hip hop Lazzybaby, ngoma yake yapili ni Magomangeta ambayo teyali amesha toa video ambayo ilitengenezwa na I com video Dir Iddi com ni video kali yaukweli ukipata bahati ya kuitazama utaona sehemu mbalimbali za mkoa wa mara.

Tuesday, September 18, 2012

WAKALI WA KAHAMA

Jamaa wanatamba sana maeneo ya kahama kaamkao wa kula wanakalibia kutoa ngoma yao mpya hivi kalibuni.

LAZZYBABY

Lazzy baby makali wa hip hop atoa video yake mpya inayokwenda kwa jina la "i will be waiting"cheki na mi kwenye blog hii au kwenye blog mpya ya matukio mbalimbali ya the track masters djs msanii huyu kwawale mlio kuwepo kwenye fiesta mwaka jana na mwaka huu alifanya maajabu mpaka baba jonh adam mchomvu alimkubali kutokana na uwezo alionao kwenye jukwaa la fiesta katiya wasanii wa hip hop mkoa wa mara yeye amekuwa nikivutio kwa vijana wa mkoa huu.

B20 BEAT AGENDA NA TBC ONE

Mzee wa chika hapa acha hapa H baba

HUYO NDO BOBAN

18 WATUA MOROGORO KUIVAA MTIBWA

baada ya kutoka sare na prison ya mbeya katika mchezo wa kwanza wa ligi soka tanzania bara kocha wa dar young afrikan ameshusha kikosi cha wachezaji 18 mjini moro kuivaa mtibwa shuga katika mchezo wa kesho huku akilalamika kuwa hajaoga siku mbili walipo kuwa mbeya kutokana na kukaa katika hoteli isiyo kuwa na kiwango walipokuwa mbeya katika mchezo wa fungua dimba.

Thursday, September 13, 2012

KAGINA NOTI ZONGOLI AJITOSA KATIKA UCHAGUZI CCM MKOA MARA


Katika mchakato wa uchaguzi ndani ya chama cha mapinduzi mkoa wa mara nae mwenyekiti wa mtaa wa kitaji D Kagina noti zongoli mwenye umri wa miaka 30 amechukua fomu ya kugombea kiti cha mwenyekiti wa mkoa wa Mara,wagombea wengine ni pamoja na Makongoro Nyerere mbunge wa Afrika mashariki na christofa chambili Kagina amewaomba vijana wenzake kumuunga mkono ili aweze kuludisha heshima ya chama na imani kwa wanachama wa ccm

FIESTA MPANGO MZIMA DODOMA NA MOROGORO

Bhaaaaaaassssssssss

JUKWAA LA SERENGRTI FIESTA 2012

SAMAKI WA MFELEJINI NYASHO MUSOMA MJINI JAMAA ANAKAMATA KWA MIKONO


anawasaka mpaka chini ya mawe nimaeneo ya barabara ya nyasho musoma mjini ni samaki aina ya mumi au watu wa pwani wanawaita kambale na baada ya kuwakamata ni biashara na mboga nyumbani kwake maisha yanasonga.

MTAALAM WA KUKAMATA SAMAKI KWA MIKONO MTALONI

anaziba upande mmoja wa mtalo ili wasimkimbie alafu anakwenda upande wa pili kavaa gam bot lakini mikononi ajavaa kitu chochote.

Wednesday, September 12, 2012

AJALI YAUA 13 MUSOMA


.








Kaimu mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa mara dr joseph nyamagwira  akitoa takwimu kwa waandishi wa habari  za watu waliofariki dunia na waliojeruhiwa .
mkuu wa wilaya ya musoma jackson msome akiwapa pole ndugu wa majeruhi na waliopoteza maisha.
Watu 13 wamefariki dunia kwa ajali ya basi dogo la abiria aina ya hiace  na wengine 18 kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya mkoa wa mara kwa matibabu zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari Kaimu Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Mara Dokta Joseph nyamagwira amesema kuwa watu 10 walifariki papo hapo baada ya gari hiyo  kupasuka tairi la nyuma na kupoteza mwelekeo na hatimaye kupinduka  mara tatu na kupoteza maisha ya wananchi.

Nyamagwira alisema watu watatu waliokuwa majeruhiwa walifariki dunia  mara baada ya kufikishwa hospitali wanaume wawili na mwanamke mmoja ,majeruhiwa wa kiume mmoja alikuwa na majeraha makubwa kichwani na mwingine alipasuka vandama na mwanamke alivunjika mbavu.

Alisema kuwa juhudi za kuwatibu  Majeruhiwa zianaendelea vizur  kwa ushirikiano wa madaktar,i isipokuwa majeruhiwa mmoja aliyevunjika mguu amepelekwa katika hospitali ya rufaa ya bugando kwaajili ya kuwekewa chuma ili aweze kupona haraka.
Gari hilo lilikuwa likitoka Musoma Mjini kuelekea butiama na ajali hiyo ilitokea eneo la nyabange nje kidogo ya manispaa ya musoma majira ya saa  kumi na mbili jioni.

Mkuu wa wilaya ya musoma Jackson msome amewatembelea majeruhi wa ajali hiyo leo na kuwahakikishia ndugu wa majeruhi kuwa serikali iko pamoja nao na serikali inahakikisha huduma zote muhimu za matibabu zinapatikana hospitalini hapo ili waweze kupona.

POLISI WAWEKA UZIBE MAANDAMANO MARA

Mwenyekiti wa mrpc akipata maelekezo ya wahariri dares salaam emmanuel bwimbo aliyeko kulia .
wanahabari baada ya kuzuiwa  maandamano na jeshi la polisi hapa wanamsubiri mwenyekiti kutoa tamko na muda mfupi mwenyekiti alitoa tamko la kutoandika habari za polisi.

WAKATI WA KEKI KATIKA BIRTHDAY YA LILIAN

huo ndio mguu wa dj mapo aliyepata ajali na kwa sasa anapata matibabu hospitali ya rufaa bugando.
hiyo ndo keki aliyoandaliwa lilian.
kushoto ni dj mapo  wa pili  dj lima  wa pili kulia lilian.
anayefungua shampeni anaitwa ruzindane.
aliyesimama baada ya birthday  kijana huyo dj mapo alipata ya ajali ya kugongwa na gari mkendo na kuvunjika mguu .


akiwalisha keki waliohudhuria hafla hiyo.