Thursday, November 29, 2012

WATU WAWILI WAFARIKI MARA

mtummoja jisia ya kiume asiyefahamika kwa jina aliuwa na wananchi wenyehasila kali baada ya kukutwa akiiba mabati toka kwenye jengo la mtu aitwaye JUMANNE KAGOSI,mnamo tarehe 29/11/2012 majira ya saa 04.00 usiku katika kijiji cha kwangwa kata ya kigera manispaa ya musoma mkoa wa mara.

akizungumza na waadishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoa wa mara S.A.C.P ABSALOM .A.MWAKYOMA amesema kuwa upelelezi unaendelea kubaini waliohusika na tukio hilo,na kuwakamata ili hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mahakamani zichukuliwe.

pia kamanda wa polisi mkoa wa mara anatoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi.

na wilayani serengeti  mugumu katika  kijiji cha soguti kata ya ikorongo tarafa ya Ngoreme bw MWITA NYAITATI CHACHA  umri wa 35,mkulima wa suguti aliuwawa kwa kukatwakatwa na mapanga kichwani
mkono wa kushoto  na mkono na mguu wa kulia na wananchi waliojichukulia sheria mkononi.

hayo yamesemwa leo na kamanda wa polisi mkoa wa mara ABSALOM .A.MWAKYOMA ofisini kwake
amesema kuwa chanzo cha tukio ni baada ya marehemu kukamatwa na ng"ombe ya wizi mali ya PHILIMON MUNDU wa kijiji cha musati uchunguzi wa tukio hilo unaendelea.

Thursday, November 22, 2012

pikipiki za kubebea wa gonjwa.zageuzwa makumbusho musoma (v)



wakati watanzania  waishio vijini wakiwa wanakosa usafiri wa ambulance ofisi ya wilaya ya musoma (v) imeifadhi nje pikipiki mpya za kubebea wagonjwa kwa muda usiojulikana nalini zitakwenda sehemu husika je nani alaumiwe?

Wednesday, November 21, 2012

pendo malima asimulia kichapo alichopata kutoka kwa mumewe

waandishi wa habari wamtembelea mkazi wa buhare pendo malima (31) aliyepata kipigo kutoka kwa mumewake na kupoteza faamu kwa siku kadhaa katika hospitali ya mkoa wa mara kushoto ni anna mroso na kulia ni shomali binda.

pendo akiwa na mama yake monica malima  wodini


beldina nyakeke.augustin mgendi na anna mrosso amesema kuwa kila mwezi uambulia kichapo kutoka kwa mumewe bwana Ndege aloys mbaye ni mvuvi ameongeza kuwa atakapo toka ataludi kijijini kwao buhemba (v).


Friday, November 16, 2012

TUME YA KATIBA YAANZA KAZI MKOA WA MARA

mkuu wa mkoa wa mara mh John tupa  akizungumza na waandishi wahabari muda mfupi uliopita ofisini kwake kuzungumzia ujio wa tume ya marekebisho ya katiba mkoani mara amesema kuwa tumehiyo itaanza kusikiliza maoniya wakazi wa wilaya ya tarime siku ya jumatatu 19/11/2012 katika katika kata ya bumare na tarime mjini na kuanzia tarehe 28/11/2012 tumehiyo itakuwa musoma mjini na itaanzia katika kata ya kitaji na nyasho,makoko na buhare tumehiyo itazunguka mkoa mzima na kumalizia wilaya ya bunda,pia mkuu wa mkoa amewaomba wanamara kuwa watulivu na kutoogopa kutoa mawazo yao juu ya katiba.

Emmanuel bwimbo wa mrpc na beldina nyakeke

maxmilia ngessi wa rfa, fazeli janja wa kulikoni na veronica wa majira,frolence wa nipashe na george marato wa itv

ghati,bigambo jeje wa( voa)  na pascal buyaga wakimsikiliza rc wa mkoa

Wednesday, November 14, 2012

WAKENYA WAZINDUA HUDUMA YA TRENI JIJI NAIROBI

Treni ya mwendokasi yazinduliwa Nairobi na raisi mwayi kibaki ya ghalimu serikali zaidi ya Ksh billion 400.

wanachuo kikuu ulia mara

makoye na wanachuo wenzake wakiwa katika maafali mjini musoma jumapili

Tuesday, November 13, 2012

VIVAA VIPYA VYA MRPC

CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MARA KIMEPOKEA VIFAA VIPYA KUTOKA UTPC.

Thursday, November 8, 2012

HALIMA MDEE NA HOJA BINAFSI BUNGENI

mbunge wa kawe kupitia CHADEMA na waziri kivuli wa aridhi na makazi Halima mdee leo ametoa hoja yake binafsi akiitaka  serikali kusimamisha mara moja zoezi la uwekezaji wa aridi wa kigeni na wa ndani kusimamishwa maramoja na kuitaka serikali kufanya uchuguzi wa udanganyifu na ubadhilifu unao fanyika kuwekwa wazi wabunge mbalimbali wanechangia hoja hio na kutoa azimio.
naye waziri mwenye dhama hiyo prof Anna tibaijuka amesema kuwa nikweli kuna ubadhilifu unaotokana na elimu kutotolewa  amesema kuwa elimu itolewe kuanzia bungeni mpaka vijijini kwani sheria ya aridhi inayo tumika sasa ni ya mwaka 1999 (4) 1999(5) na sheria ya 1962 pia waziri ametoa azimio kuwa swala la kusimamisha ugawaji wa aridi usisimamishwe ila taarifa ziwasilishwe ili kupata ufumbuzi wakina.


siku ya walipa kodi mkoani mara

katibu wa chama cha wanahabri berdina akipokea kombe baada ya timu ya wahandishi wa habari kuibuka kidedea kwa kuifunga timu ya TRA mabao 2-1  

mwanafunzi wa mwenbeni secondri akipokea zawadi baada ya kuwa mshidi wa maswali mbalimbali kuhusu TRA.

kamanda g.marato akipokea zawadi kwa niaba ya ITV.

armasi kutoka TBC 1 nayeakipokea zawadi.
mgeni rasmi wa sherehe hiyo ameshukulu kusikia TRA imevuka marengo kwa kufikisha shilingi bilion 23 kuanzia july 2012 mpaka 0ct na malengo yalikuwa ni sh bilion 22 tu pia amesema kuwa TRA watafute mbinu mbala ya ukusanyaji wa kodi ya mamapato,ametoa pongezi kwa mwekezaji wa mugumu serengeti grumet kuwa mshindi wa jumla kwa miaka miwili mfululizo pia wilaya iliyo ongoza kwa kukusanya kodi ya mapato ni wilaya ya tarime.
meneja wa TRA mara akisoma taarifa mbele ya mgeni rasmi.