Friday, January 11, 2013

UFARANSA TAYALI KUTOA MAJESHI YAKE MALI


Maandamano ya wananchi wanaotaka usalama Mali 

Wapiganaji wa Mali walioteka mji mwingine mpya wa Konna


Rais wa Ufaransa Francois Hollande, amesema nchi yake iko tayari kusaidia jeshi la Mali 
kupambana na waasi wanaodhibiti Kaskazini mwa nchi.
Amesema kuwa ataweza kujibu haraka ombi kwa serikali yake la kutoa msaada wa kijeshi kwa nchi hiyo ili kusitisha harakati za wapiganaji hao.
Lakini alisema kuwa wataweza tu kufanya kazi yao ikiwa Umoja wa Mataifa utawaidhinisha. Umoja wa Matifa hata hivyo ndio umetoa wito wa kupelekwa kwa wanajeshi wa kimataifa nchini humo katika mkutano wa dharura wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.
Rais Hollande, alisema kuwa harakati za wapigajani hao wanaohusishwa na kundi la Al Qaeda,sasa zinatishia utahbiti wa Mali. Hadi sasa Ufaransa imesema iko tayari tu kutoa mafunzo kwa jeshi la Mali.
Awali baraza la usalama la Umoja wa mataifa lilitoa wito wa kupelekwa kwa wanajeshi wa kimataifa nchini humo ambako wapiganaji wa kiisilamu wanadai wameuteka mji muhimu wa Konna.
Wakati huohuo, duru za kidiplomasia zinasema kuwa rais wa nchi hiyo ametoa wito kwa Ufaransa kusaidia katika kupambana na wapiganaji hao, hoja iliyojadiliwa katika mkutano wa dharura wa baraza la usalama la umoja wa mataifa.

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Susan Rice, alihoji ikiwa rais Dioncounda Traore alikuwa ametoa ombi maalum na kufafanua aina ya msaada anaotaka.
Wapiganaji wa Mali walioteka mji mwingine mpya wa Konna
Mwezi jana Umoja wa Mataifa uliidhinisha mpango wa kutuma wanajeshi elfu tatu kuweza kutwaa eneo la Kaskazini mwa nchi ambalo linadhibitiwa na makundi ya kigaidi yaliyo na uhusiano na kundi la Al Qaeda.
Wapiganaji wa kiisilamu wameweka sheria kali za kiisilamu katika eneo hilo.
Kwa sababu ya mipango ya usafiri na vifaa , kikosi cha wanajeshi wa Afrika hakitatarajiwa kuanza kazi hadi ifikapo Septemba au Oktoba.
 .........................................................................................................

Waasi Jamuhuri ya Afrika ya Kati wasitisha vita

 

 
 
Rais wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Francois Bozize akiwahutubia waandishi wa habari

Kiongozi wa waasi wa Seleka


Waasi wanaopambana na serikali katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, wanasema kuwa wamekubaliana kusitisha mapigano kwa wiki moja baada ya mazungumzo ya amani nchini Gabon.
Waasi wanasema kuwa wanataka wanajeshi wa Afrika Kusini waondoke nchini humo na pia serikali iwaachilie wafungwa wa kisiasa ili waweze kuafikia mwafaka wa pamoja.
Waasi hao wa 'Seleka' walidhibiti maeneo ya Kaskazini na Mashariki kwa CAR katika kipindi cha wiki nne kuanzia Disema mwaka jana.
Wanamtuhumu rais Francois Bozize kwa kukiuka mikataba kadhaa ya amani ambayo walitia saini.

''Tutakubaliana kimsingi kutopigana kwa wiki moja'' alisema msemaji wa kundi hilo, Florian Ndjadder.

Aliongeza kuwa mwafaka utaweza kuruhusu waasi kuona ikiwa serikali itaweza kujitolea kupata suluhu kwa mzozo huu na kutimiza matakwa yao.
Waasi hao ambao wamekuwa wakimtaka rais kujiuzulu, pia walisema kuwa wanataka waziri mkuu mpya kuteuliwa kutoka kwa upinzani na hata kutoa madai zaidi.

" Mamluki hao kutoka Afrika Kusini lazima waondoke Jamuhuri ya Afrika ya Kati, wafungwa wa kisiasa lazima waachiliwe bila vikwazo wakati huohuo,'' alisema bwana Ndjadder.
Afrika Kusini imeanza kutuma wanajeshi 400 kusaidia kudhibiti hali katika Jamuhuri ya Afrika ya kati. Wanajeshi kutoka nchi jirani pia wameweza kutumwa huko. Ufaransa na Marekani wamekataa ombi la serikali kusaidia katika kupambana na waasi hao
......................................................................................................
 

Bunge jipya lililokarabatiwa kwa zaidi ya dola milioni kumi
Wabunge nchini Kenya wamejizawadia

Wabunge nchini Kenya wamejizawadia dola 107,000 kama marupurupu katika mojawpao ya vikao vyao vya mwisho vya bunge hilo kabla ya uchaguzi mkuu kufayika mwezi Machi.
Kila mbunge ataweza kupata mlinzi wa maisha, pasi ya kidiplomasia na kupata huduma za juu zaidi katika viwanja vye ndege kote duniani. Haya ndiyo mapendekezo yaliyo katika mswaada waliopiitisha ukisubiri kuidhinishwa na rais Mwai Kibaki
Ni mara ya pili wabunge wamepitisha mswaada huu wa kujizawadia mwishoni mwa vikao vyao vyabunge . Rais Mwai Kibaki alitupilia mbali mswaada wa kwanza kama huu ambao ulizua ghadhabu miongoni mwa wananchi.

Wabunge wa Kenya ni miongoni mwa wabunge wanaopokea mishahara ya juu zaidi barani Afrika kila mmoja akipata dola elfu kumi na tatu kila mwezi.
Lakini mshahara wa mkenya wa kawaida ni takriban dola 1,700 kila mwezi.
Mswaada huu, ulipitishwa siku ya Jumatano na wabunge chini ya thelathini waliokuwa bungeni. Walikarabati bunge lao kwa kutumia dola milioni kumi na mbili kulingana na stakabadhi za bunge zilizotolewa hapo jana.

Malipo haya ni sawa na yale yaliyokuwepo katika mswaada walioupitisha mwezi Oktoba, lakini wakati huu wabunge hao pia wamependekeza marupurupu kwa rais ambaye atalipwa dola laki tatu sawa na makamu wa rais na waziri mkuu.

Alipotupilia mbali mswaada wa kwanza , Rais Kibaki lisema kuwa haiwezekani kwa wabunge kulipwa mamilioni ya dola wakati uchumi ungali umedumaa.
Tume ya kushughulikia mishahara ya wafanyakazi wa umme, iliambia wakenya kuwa hakuna uhakika ikiwa hatua yao inakuika katiba.

Mashirika ya kutetea haki za kibinadamu yameelezea kukerwa sana na hatua ya wabunge. Tayari waziri mkuu Raila Odinga amepinga mswaada huo akisema kuwa ni kama uhalifu dhidi ya wakenya na kwamba anashauriana na rais Mwai Kibaki kuhusu hatua itakayokuwa sawa kwa wakenya. 
.......................................................................................................
 



No comments:

Post a Comment