Monday, January 21, 2013

MATEKA WALIOUAWA ALGELIA WAONGEZEKA

 


                         Wanajeshi wa Algeria wadhibiti uwanja wa Ndege mjini Ain Amenas
 

                             Kiongozi wa wapiganaji wa kiisilamu Algeria Mokhtar Belmokhtar

 Wanajeshi wanaendelea na upekuzi katika eneo kulipotokea utekaji nyara katika kiwanda cha mafuta cha Amenas. Ndani ya kiwanda hicho zaidi ya maiti ishirini zilizoteketea kiasi cha kutoweza kutambulika zilipatikana.
 Kufikia sasa idadi ya waliofariki katika kisa hicho imefikia 80.
Hata hivyo, bado haijabainika ni wangapi miongoni mwa waliopfariki walikuwa mateka
Taarifa zaidi zinarifu kuwa Maiti za mateka kutoka Japan, Norway, Uingereza, Marekani na Malaysia bado hazijatambuliwa huku maafisa wa usalama wakisema kuwa watekaji nyara watano tayari walithibitishwa kuuawa na wapiganaji.
Takriban mateka 48 wameaminika kuuawa katika siku nne za sokomoko kwenye kiwanda cha gesi nchini Algeria.
Wanamgambo 5 inaarifiwa walikamatwa hiyo Jumapili
Maafisa wa utawala awali walisema Jumamosi kuwa watekaji nyara 32 waliuawa.
Hata hivyo makomando waliweza kumaliza vurugu hilo siku ya Jumamosi. Maafifa walisema kuwa idadi kamili ya watu waliofariki itatolewa baadaye.
Jeshi lililazimika kufanya operesheni hiyo baada ya wanamgambo hao kuanza kuwaua mateka.
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron na rais wa Marekani, Barack Obama, wamelaumu magaidi kwa kusababisha vifo vya mateka.
Kiongozi wa wapiganaji wa kiisilamu Algeria Mokhtar Belmokhtar
Kingozi wa wapiganaji hao, Mokhtar Belmokhtar, alisema kuwa wako tayari kufanya mazungumao na serikali ya Algeria lakini sharti wakome kushambulia wapiganaji wa kiisilamu nchini Mali.
Na Jumapili, waziri wa ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian, alitaja kitendo cha wanamgambo hao kama kitendo cha vita.



               Ufaransa wadhibiti Diablay




                                                 Harakati za jeshi la kigeni nchini Mali
  
Wanajeshi wa Ufaransa na wa Mali, wameingia katikati mwa mji wa Diabaly, bila ya makabiliano yoyote na wapiganaji wa kiisilamu.
Msururu wa magari 30 ya kijeshi yaliyokuwa yamewabba wanajeshi 200 wa Mali na Ufaransa, yalionekana yakielekea mjini humo.
Wapiganaji walitoroka Ijumaa baada ya mji huo kushambuliwa kwa ndege za kijeshi
Ufaransa ilianza operesheni yake ya kijeshi dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu nchini Mali wiki moja iliyopita ili kujaribu kuwaondoa wapiganaji wanaodhibiti Kaskazini mwa Mali.
Jeshi la Ufaransa linanuia kuweza kudhibiti eneo hilo kikamilifu kutoka kwa wapiganaji wa kiisilamu. Hii ni kwa mujibu wa waziri wa ulinzi wa Ufaransa,Jean-Yves Le Drian.
"hatutaondoka bila ya kuwafurusha kabisa wapiganaji hao, '' waziri aliambia vyombo vya habari.
Ufaransa imetuma takriban wanajeshi 2,000 kusaidia Mali kupambana na wapiganaji hao wa kiisilamu.


              Muasi wa Nigeria hatiani A. Kusini





                                          Henry Okah kiongozi wa kundi la waasi la Mend
Mahakama nchini Afrika Kusini imempata na hatia ya vitendo vya kigaidi kiongozi wa waasi wa Nigeria Henry Okah.
Okah anasemekana kupanga mashambulizi ya mabomu yaliyotegwa ndani ya gari na kuwaua watu 12.
Okah alipatikana na hatia ya makosa 13 kuhusiana na vitendo vya kigaidi.
Alikamatwa mjini Johannesburg siku moja baada ya mabomu mawili kulipuka wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka 50 ya uhuru wa Nigeria.
Alikanusha makosa hayo ingawa kundi analoongoza la Mend, lilikiri kutekeleza mashambulizi hayo.
Jaji wa mahakama kuu mjini Johannesburg, Neels Claassen, alimpata na hatia Okah ya makosa ya kupanga njama ya mashambulizi pamoja na kufanya vitendo vya kigaidi ikiwemo kulipua mabomu.
"ushahidi ambao ulitolewa na washirika wake haukupingana,'' alisema jaji Claassen
Okah alikamatwa kwa kosa la kumiliki bunduki kinyume na sheria nchini Angola mwaka 2007 na kisha kuhamishwa hadi nchini Nigeria ingawa hakuwahi kuhukumiwa.
Aliachiliwa baada ya miaka miwili chini ya msamaha uliotolewa kwa wapiganaji walio katika maeneo ya mafuta na ndipo aliporejea Afrika Kusini ambako aliishi hadi mwaka 2003.



No comments:

Post a Comment