Thursday, October 25, 2012

MAGUFULI AKUBALI OMBI

makabidhiziano yafanyika mbele ya waziri mwenye dhamana.

baada ya makabiziano hayo ndipo Mh magufuli alipo toa tamko kwa kuiomba kamati ya ulinzi ya mkoa kutoa ushilikiano ili kudhibiti wizi unaofanyika katika miladi malimbali ya wachina hapa nchini mbele ya mbunge wa morogoro kusini Mh innocent kalgeria aliye kushoto na kulia ni balozi mrago pia alikubali ombi la kutumia wakandalasi wazawa katika miladi mingine,maladi huo utachukua miezi 24 tu.

mhandisi patrick mfukule kushoto na mtendaji mkuu kutoka kampuni ya ujenzi ya china raylway 15 Bureau group corporation (CR15G) Zhang tonggang (kulia) wakiweka saini.

Tuesday, October 16, 2012

BURIANI KAMANDA BARLOW


enzi ya uhai wake mpoka siku ya mwisho.

WAJUMBE WA CCM MWANZA WAPATA AJALI LEO



Wajumbe wa ccm wilaya ya misungwi leo hii wamepata ajali maeneo ya buhongwa iliyopo katika wilaya nyamagana walipo kuwa wakielekea katita uchaguzi mkuu ngazi ya mkoa wa mwanza majira ya saa 3.00 za asubuhi ambapo deleva wa basi hilo amepoteza maisha hapo hapo na wajumbe takriban saba nimajelui wako katika hospitali ya bugando kwa matibabu zaidi.


chanzo cha ajali hio ni basi hilo lilikuwa likikwepa loli aina ya fuso ambalo lilikuwa likigeuka kujiweka sawa kuingia barabarani  ndipo basi hilo likiwa katika mwendo kasi liligoga fuso na kupinduka papo hapo,wajumbe hao walikuwa safarini jijini mwanza katika uchaguzi wa wajumbe wa halmashauri kuu ya ccm mkoa wa mwanza unaofanyika leo katika uwanja wa ccm kirumba.

MH MAKONGORO NYERERE ANENA

likuwa ni siku moja tu kabla ya kumbukumbu ya mwl juliasi .k. nyerere, mkoani mara kulikuwa na uchaguzi wa mwenyekiti wa ccm ngazi ya mkoa wa mara ambapo wagombea walikuwa ni mh chambili,mh makongoro na mh sanya  ilibidi kura kuludiwa mara mbili baada ya wagombea kutovuka nusu ya kura za wajumbe walio kuwepo hapo ukumbini. baada ya kuludiwa mshindi aliibuka mh sanya kutoka wilayani bunda wapili alikuwa ni mh makongolo alikukubaliana na matokea ya kura ila alitoa wito kwa mwenyekiti mpya kwamba avunje makundi ndani ya chama ilikuleta umoja na mshikamano heshima ndani ya chama.

Friday, October 5, 2012

ZIWA VICTORIA NIKIVUTIO MUSOMA


unapokuwa musoma mjini ususani maeneo ya makoko seminari ndiyo unaweza kutazama jinsi ziwa linavyo onekana vizuri, kwambali nimajali ya mawe ambapo juu kunamnala ambao uliwekwa tokea enzi za utawala wa hawamu ya kwanza wakati bandali ya musoma ilipo kuwa inatumika kwa meli za mizigo na abilia lakini sasa hivi bandari hiyo ni sehemu ya popo,pimbi,njiwa na mapango ya wahalifu, kwenye mlima huo kulikuwa kuna taa nyekundu huwaka usiku ili kuiongoza meli kama ikiwa inatokea mwanza,kampala au kisumu sasa hivi hata mnala wenyewe sidhani kama hupo.

vilevile kwaupande wa kulia ukiwa maeneo hayohayo ya makoko beach utakiona kiwanda kikubwa sana cha minofu ya samaki wanaovuliwa katika ziwa hilo na minofu yake kuuzwa ulaya nikiwanda cha mwekezaji kutoka kenya kinajulikana kwa jina la BUKANGA bado kinaendelea kufanya kazi japo kwa kusuasua sidhani kama kinatoa huduma zamani.


hapo sio polini ni kisiwa cha RUKUBA BEACH ambapo kuna hotel ya kitalii iliyo jengwa zamani kidogo kuna ndani yake kuna vijiji kadhaa kuna Rukuba ndago ambapo pamoja na kuwepo mwekezaji na hotel hiyo pia wakazi wa hapo ni wavuvi wa dagaa na samaki sato na sangara wanao letwa kiwandani bukanga kila siku, kuna rukuba centani na hesaru wavuvi wengi utokea huko.


kiwanda cha samaki BUKANGA.


Dagaa wanao vuliwa na wakazi wa maeneo hayo ya MAKOKO BEACH huanikwa kila siku alfajili na jioni kuwekwa kwenye majunia kwaajili ya safari ya Dar,Arusha,Tunduma na nk dememja sh 3000 adi sh 5000 kutokana na hali yahewa itakavyo kuwa.