Thursday, December 13, 2012

mtu adondoka kwenye ndege london

 
Picha ya mtu aliyeanguka kutoka kwenye ndege wakati inatua jijini London.
POLISI wa Jiji la London, Uingereza, bado wanahangaika kujua uraia wa mtu mmoja wanayeamini alitoka Afrika na ambaye alianguka na kukutwa amekufa baada ya ndege moja kufungua milango ya magurudumu yake wakati inataka kutua uwanja wa Heathrow mwezi Septemba mwaka huu.

Polisi hao wana picha ya mtu huyo iliyotayarishwa kwa kompyuta.

Vilevile, wachunguzi wanaamini mtu huyo anaweza kuwa alikufa muda mfupi tu baada ya ndege kuondoka ardhini ilikotokea, kutokana na kukosa hewa na kupigwa na ubaridi mkali wakati ndege ikiwa juu, hususani kwa vile alikuwa amejichimbia sehemu yanakoingia magurudumu ya ndege.

No comments:

Post a Comment