Saturday, December 29, 2012

MAUAJI YA BODABODA

MADEREVA WA PIKIPIKI WAKIPITA KATIKA BARABARA YA MKENDO KWENDA KUMSHUHUDIA MWENZAO HOSPITALI YA MKOA WA MARA

SEHEMU YA MGUU AMBAO PIA ULIKATWA NA MAPANGA  

BODABODA WAKIWA NJE YA HOSPITALI YA MKOA WA MARA

MWENZAO ACHINJWA


Mbunge atangaza vita na Nyani waharibifu

          -Mwananchi atakayeua nyani na kumpelekea mkia kulipwa elfu kumi



Mbunge wa Jimbo la Kibara Kangi Lugora (CCM) ametangaza vita na Nyani ambao amedai wamekuwa wakiharibu mazao ya Wananchi mashambani na wengine kuwadhuru watu katika maeneo yao ya makazi na kupelekea kukwamisha shughuli za kiuchumi zinazofanywa na Wananchi katika Jimbo hilo.

Akizungumza na BLOGU HII Mjini Bunda Kangi alisema tayari walishatoa taarifa Serikalini kupitia Wizara ya Mali Asili na Utalii kuhusiana na uharibifu unaofanywa na Nyani hao lakini wamekuwa kimya bila kuchukua hatua zinazostahili hivyo amaeamua kuwahamasisha Wananchi katika Jimbo lake kuhakikisha wanawaangaamiza Nyani wote katika maeneo yao.

Alisema nyani hao wamekuwa wakifanya uharibifu mkubwa ambao wameshindwa kuuvulia wakati walishatoa taarifa katika sehemu zinazohusika na kukaliwa kimya hivyo wameamua kwa nguvu zao kuhakikisha wanapambana na nyani hao na kuwaondoa kabisa katika maeneo yao.

Mbunge huyo alisema amewaajili watu watano ambao wanatumia siraha za bunduki na kijadi kuhakikisha popote wanakutana na nyani  kuwaua ili wasiendelee kuharibu mazao ya Wananchi na kuwadhuru binadamu kwa kuwa Serikali imeshindwa kulichukulia hatua suala hilo.

Alisema licha ya kuwaajili watu hao pia amewatangazia ajira Wananchi wa Jimbo hilo kwa yeyote atakaye ua nyani na kisha kumpelekea mkia atapewa shilingi elfu kumi papo hapo kwa kuwa amewaweka mawakala ambao wanatumia stakabadhi ambazo zimeandaliwa kwa kazi hiyo ya kuwalipa Wananchi.

"Hatuwezi kuendelea kukubaliana na hali hii ya kuharibiwa mazao yetu huku Serikali imekaa kimya tutawaua nyani wote kwa kuwa hawana faida kwetu na nimeshaandaa fedha za kutosha ambazo kila Mwananchi atakayefanya kazi hiyo atapata malipo yake,"alisema Kangi.

Alisema nyani hao wamekithiri sana katika milima ya Lagata,Ilamba na Kitengere ambapo amedai huko kote amewaweka mawakala ambao watahakikisha kila Mwananchi atakayepeleka mkia wa nyani anapata malipo yake papo hapo pasipo usumbufu.

"Kwanza nyani hawa sio utalii kwetu na hakuna mtu yeyote anayekuja hapa kufanya utalii wa kuangalia nyani na kama Serikali ingeona wanafaa kwa utalii wangesikiliza vilio vya Wananchi kutokana na adha wanayoipata ya kuharibiwa mazao yao na kuwadhuru Wananchi,"alisema Mbunge huyo. 

Mbunge Kangi aliongeza kuwa licha ya uharibifu wa nyani hao lakini pia kumekuwepo na matukio ya Wananchi kudhuliwa na Mamba pamoja na Viboko katika Ziwa Victoria ambapo pia wameanzisha vita ya kuhakikisha wanawawinda mamba pamoja na viboko na kuwaua.

Alisema hadi sasa watu wanne wameuwawa na mamba pamoja na viboko huku Serikali ikikaa kimya hivyo wao wameamua kuanzisha mapambano ambayo yatawaangamiza mamba na vibiko wote ambao wamekuwa wakiwadhuru Wananchi. 

.....................................................................................................................................

    Profesa Muhongo aijibu CUF kuhusu mgawo wa umeme



WAZIRI wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amesisitiza kuwa hakuna hoja ya mgawo wa umeme kwa sasa hapa Nchini kutokana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kujipanga kutafuta vyanzo vingine vya uzalisha mbadala wa umeme kuliko kutegemea maji ili ifikapo Mwaka 2013 Tanzania iweze kupata umeme wa uhakika.

Kauli hiyo ameitoa Mjini hapa katika kikao kilichowashilikisha Vijana wa Manispaa ya Musoma kutaka kujua ni changamoto gani zinazopelekea Mji huo kukosa Maendeleo na kuzungummzia jinsi Shirika hilo linavyoendeleaa kufanya mabadiliko katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi na kupata umeme wa uhakika.

Alisema anapingana na maazimio yaliyotolewa na Chama cha Wananchi (CUF) katika Baraza lake Uongozi lilofanyika hivi karibuni Jijini Dar es salaam na kueleza kuwa upo mgawo usio rasmi wa umeme ambao unapelekea kero kwa Wananchi na kukwamisha shughuli za kimaendeleo ambazo zinahitaji nishati ya umeme.

Profesa Muhongo alisema suala la kukatika kwa umeme kwa dakika mbili ama tatu sio mgawo kama inavyoelezwa na Chama hicho bali ni kutokana na miundombinu ambayo imechakaa ambapo kwa sasa Tanesco imeelekeza katika kufanya jitihada za kuibadilisha ili kuweza kukabiliana na changamoto hiyo.

''Sote tunafahamu miundombinu ya Shirika hili mingi imechakaa na inahitaji mabadiliko ambayo kwa sasa kwa asilimia kubwa inafanyiwa kazi hivyo inapelekea kuwepo na kero ya kukatika kwa umeme kwa muda furani lakini sio kila siku na huo sio mgawo wa umeme jamani tuache propaganda za kisiasa katika masuala mengine ya maslahi ya Taifa,"alisema Muhongo.

Alisema yeye akiwa kama Waziri mwenye dhamana ya umeme atamueleza Waziri Mkuu ama Rais iwapo kutakuwa na mgawo wa umeme lakini sio watu kusimama na kusema kuna mgawo kitu ambacho amekiita ni uzushi ambao unatumiwa na wanasiasa katika propoganda zao ambazo hazina tija kwa Taifa.

Alidai Tanesco inajipanga kuhakikisha umeme wa uhakika unapatikana na tayari imeanza programu ya kusambaza umeme Nchi nzima katika Vijiji na Wilaya na kusema kazi hiyo inahitaji kupana ushirikiano katika kuifanukisha na kuomba kupata maoni kwa kila Mwananchi namna ambavyo anataka shirika hilo lifanye katika kuleta ufanisi tofauti na kipindi cha nyuma

Aidha Profesa Muhongo alisema zipo changamoto nyingine ambazo zinafanywa na watu wasio wazalendo kwa kuiba mafuta ya Transifoma pamoja na waya za umeme hali inayopelekea kujitokeza kwa matatizo ya kukatika kwa umeme ili kupisha mafundi kuweza kurekebisha na kurudisha umeme na kuwaomba Wananchi kuweza kutoa taarifa pale wanapoona mtu anataka kuhujumu shirika hilo.

Akizungumzia masuala ya kimaendeleo katika Mji wa Musoma,Waziri Muhongo aliwataka vijana wa Mji huo kuacha ubinafsi na kushirikiana katika kujitafutia Maendeleo na kubadilisha muonekano wa Mji huo na kusisitiza kujiepusha na kukalia siasa muda wote bali wajishughulishe na shughuli mbalimbali za kujiletea maendeleo.
 

.................................................................................................................................

                          Amuuwa mtoto kwa kumchapa fimbo


MKAZI mmoja wa kata ya Nyasho katika Manispaa ya Musoma aliyefahamika kwa jina la Yohana Msafiri (38) amemuuwa mtoto wake Veronica Yohana kwa kumchapa na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake Desemba 23 na kupelekea kifo chake akiwa njiani kupelekwa hospitali baada ya kuzidiwa na maumivu.

Katika taarifa yake kwa Vyombo vya Habari,Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mara Absalom Mwakyoma  alisema tukio hilo lilitokea majira ya saa 5 usiku katika maeneo hayo ya Nyakato ambapo chanzo cha kuchapwa viboko kwa mtoto huyo na matatizo ya kifamilia.

Alisema mzaza wa Mtoto huyo anashikiliwa na Jeshi la Polisi kutokana na tukio hilo ambapo amedai mara baada ya kukamilika kwa upelelezi mzazi huyo atafikishwa Mahakamani kuweza kujibu tuhuma zinazomkabili.

Kutokana na tukio hilo Kamanda Mwakyoma amewataka wazazi kuangalia adhabu mbadala ambazo wanaweza kuwapa watoto pale wanapokuwa wanafanya makosa katika kuwafunza na sio kuwa na hasira ambayo inaweza kupelekea madhara mengine makubwa zaidi.

"Wazazi lazima waangalie adhabu mbadala ambazo zinapaswa kupewa watoto pale wanapofanya makosa maana kwanza ifahamike hawa ni watoto na yaale wanayoyafanya ni kutopkana na utoto wao hivyo iwepo busara katika kutaka kutoa adhabu kwa watoto wetu,"alisema Kamanda Mwakyoma.

Katika tukio lingine Kamanda huyo wa Jeshi la Polisi Mkoani Mara alisema mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Gogogo anayekadiliwa kuwa na umri kati ya m,ika 40 na 45 mkazi wa Bunda aliyekuwa akiishi kata ya Nyakato Mshikamano katika Manispaa ya Musoma aliuwawa kwa kushambuliwa na kuchomwa moto kwa kudaiwa anahusika katika matukio ya ujambazi.

Kamanda Mwakyoma alisema Wananchi wanapomuhisi mtu anashiliki katika matukio ya uhalifu ni vyema kutoa taarifa Polisi na si kujichukulia sheria mkononi kwani hata kama mtuhumiwa anashiliki anapokamatwa anaweza kutoa taarifa ambazo zinaweza kuwapata watu wengine ambao anashiliki nao katika matukio hayo.

Alisema kujichukulia sheria mkononi ni kosa kwa mujibu wa sheria na atakaye kamatwa kutokana na kosa la kujichulia sheria mkononi atafikishwa Mahakamani kutokana na kosa hilo na kutoa tahadhari kwa Wananchi kuacha tabia hiyo kwani haifai na sheria hairuhusu kujichukulia sheria mkononi.

....................................................................................................................................






     

Thursday, December 20, 2012

BODABODA MUSOMA ACHINJWA

WANANCHI WAKISHUHUDIA MWILI WA BODABODA ANYEDAIWA NI MKAZI WA KIGERA KIARA ALIYECHINJWA NA KUNYANG'ANYWA PIKIPIKI


Thursday, December 13, 2012

mtu adondoka kwenye ndege london

 
Picha ya mtu aliyeanguka kutoka kwenye ndege wakati inatua jijini London.
POLISI wa Jiji la London, Uingereza, bado wanahangaika kujua uraia wa mtu mmoja wanayeamini alitoka Afrika na ambaye alianguka na kukutwa amekufa baada ya ndege moja kufungua milango ya magurudumu yake wakati inataka kutua uwanja wa Heathrow mwezi Septemba mwaka huu.

Polisi hao wana picha ya mtu huyo iliyotayarishwa kwa kompyuta.

Vilevile, wachunguzi wanaamini mtu huyo anaweza kuwa alikufa muda mfupi tu baada ya ndege kuondoka ardhini ilikotokea, kutokana na kukosa hewa na kupigwa na ubaridi mkali wakati ndege ikiwa juu, hususani kwa vile alikuwa amejichimbia sehemu yanakoingia magurudumu ya ndege.

Tuesday, December 11, 2012

MAAJABU YA AFRICA MASHARIKI

NAIROBI KENYA

MOMBASSA KENYA

NAIROBI KENYA

MOUNT LONGNOT KENYA

MOMBASSA

KENYA MOMBASSA RAHA
GIRAFFE SKYLINE NAIROBI

hilton hotel nairobi

nyari brigd nairobi

nyanya yake obama bibi sala obama

Monday, December 10, 2012

WAZEE NA WASAAFU WA WILAYA NA MKOA WA MARA WANENA


Baada ya mbunge wa musoma mjini kupitia chama cha maendeleo CHADEM MH 
VICENT NYERERE , jana kutoa tamko kuhusu matukio mbalimbali yanayodaiwa kutokea mkoni hapa Wataafu Viongozi wa vyama vya Siasa na Serikali, Wachungaji na Mashehe Wilaya ya Musoma, Mkoa wa Mara wamekanusha vikali taarifa zilizochapishwa kwenye baadhi ya magazeti na Televisheni nchini kuwa ndani ya wilaya hiyo watu 17 wakiwemo wanawake 5 wamechinjwa kati ya Oktoba hadi Desemba mwaka huu.

Wazee hao pia waliiagiza Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya hiyo kumkamata mwandishi wa habari hizo ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria kutoa ushahidi wa watu waliochinjwa kisha kumfikisha mahakamani kujibu mashitaka ya kuandika habari za uzushi na uchochezi na kuwatia hofu wananchi.

Wakizungumza na Mkuu wa Wilaya hiyo Jackson Msome na kamati yake ulinzi na usalama kwenye kikao cha dharura kilichofanyika kwenye ukumbi wa chuo cha Waganga katika Manispaa hiyo wazee hao kwa kauli moja walimuhakikishi Mkuu wa wilaya hiyo kuwa habari hizo ni za uzushi zenye kuwatia hofu wananchi.

“Ukisoma kwenye haya magazeti utagundua habari hii imekaa kisiasa kwani hata Mbunge wa Chadema Vicent Nyerere anadiriki kusema kuwa anamtaka IGP said Mwema akomeshe mauaji hayo pia kamati ya ulinzi na usalama imekalia siasa huu ni uzushi na tunapinga kama kuna ukweli tunaomba otoe ushahidi kwa kuonyesha maiti zilizochinjwa,”alisema Mzee Seleman Kerenge.

Alisema kuwa vyombo hivyo vya habari vinalengo vya kuvuruga hali halisi ya amani na usalama ndani ya mji wa Musoma na kudai kuwa hakuna mtu yeyote aliwahi kuchinjwa ndani ya Manispaa hiyo.

Mzee Abdu Husein wa Makoko alisema kuwa wazazi wengi nchini hawapendi kutoa matatizo ya watoto wao hata kama wanashiriki katika vitendo viovu ambapo wanazua matatizo makubwa kwenye jamii.

“Tuna mapungufu makubwa sisi kama wazazi hata kama unajua matatizo ya vijana wako hutaki kusema ukweli, wazazi wengi hata vikao na vijana wao hawafanyi, tuna mamlaka lakini hatuyatumii,”alisema Husein kwa hasira kubwa.

Akitoa taarifa mbele ya wazee na mkuu wa wilaya Kaimu kamanda wa Polisi katika wilaya hiyo Lucas Hupa alisema kuwa matukio ambayo yalitokea katika kipindi cha mwezi Oktoba na Novemba ni matatu.

Alisema kuwa tukio la kwanza lilitokea Oktoba 19, Enock ambaye
alikuwa mlinzi alifariki dunia katika Hospitali ya Mkoa wa Mara baada ya kukatwa kwa mapanga na watu wanaodaiwa kuwa majambazi.

Tukio la pili lilitokea Oktoba 28, mwaka huu ambapo Msichana Lilian Bonifance (12) aliuawa na watu wasiojulikana na mwili wake kutupwa na tukio la mwisho lilitokea Novemba 21 ambapo mlinzi wa kampuni ya ulinzi ya Salama aliuawa na watu wanaodai kuwa majambazi.

Hupa alisema kuwa tayari jeshi hilo linawashikilia watu 16 na
watuhumiwa nane walisomewa mashitaka ya mauaji na kupelekwa magereza.

Naye Mkuu wa Wilaya Msome alisema kuwa kuna matukio yapo ndani ya wilaya hiyo lakini sio kama inavyozungumzwa kwa sasa ambapo ni hali ya kuwatisha wananchi wa Manispaa hiyo.

“Waandishi wa habari ni ndugu zetu wote tunafanya kazi kwa kuwatumikia wananchi tuache kuandika habari za uzushi na uchochezi ambazo zinatia hofu wananchi wetu,”alisema Msome.

Msome alisema kuwa Waandishi wa habari hawajaitendea haki Manispaa hiyo kutokana na habari hiyo ambayo alisema kuwa ni ya uzushi na kuwaomba kuandika habari sahihi ambazo hazipotoshi umma.

“Madhumuni ya vyombo vya habari na kazi ya mwandishi wa habari ni kufundisha, kuburudisha na kuelimisha sio kupotosha na kuchochea hayo sio maaili ya uandishi wa habari,”alisema.

Baada ya ukanushaji wa mauaji hayo Msome amewaomba wazee, Viongozi naViongozi wa dini kushirikiana na kuanzisha ulinzi shirikishi ili kuepukana na uzushi kama huo uliotokea ambapo ataanza na mafunzo juu ya ulinzi huo ambao yataanza Desemba 13 mwaka huu kwa kata nne za Iringo, Mkendo, Kitaji na na zingine zitafuata.

Taarifa ambazo hivi karibuni zilitolewa na Jeshi la Polisi Mkoa wa
Mara kupitia kwa Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa huo, Japhet Lusingu kuwa ni matukio mawili ya watu kuchinjwa ndiyo yaliyoripotiwa na yalitokea katika Wilaya ya Butiama na sio watu 17 kama ilivyotangazwa.

Tukio la kwanza ni mwanawake aliyetambulika kwa jina la Blandina Peru (28) mkazi wa kijiji cha Mahare, kata ya Etaro aliuwawa Desemba 2 mwaka huu kwa kukatwa koromeo na kubakwa na wauaji kabla ya kumuua wakati akiwa porini akikata kuni na watuhumiwa wa tukio hilo bado hawajakamatwa.

Tukio la pili lilitokea Kijiji cha Kabegi, Kata ya Nyakatende, Wilaya
hiyo hiyo ambapo Sabina Mkireri (44) mkazi wa kijiji cha kiemba
aliwawa kwa kuchinjwa shingo na kichwa chake kuchukuliwa na watu wasiojulikana katika kijiji cha kabegi na watu sita wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano.

MBUNGE WA MUSOMA MJINI


 
    MH MBUNGE WA MUSOMA MJINI KUPITIA CHADEMA VICENTI KIBOKO NYERERE
wananchi wengi wa jimbo ilo walijitokeza kwa wingi katika viwanja vya shule ya msingi mukondo musoma mjini MH VICENT NYERERE aliambatana na aliyekuwa mbunge wa ARUSHA mjini MH GODBLES LEMA .

Katika Mkutano huo ambao ulimalizika kwa Wananchi kuwasindikiza kwa msururu Mkubwa kutoka katika viwanja hivyo hadi katika makao makuu ya Chama hicho Wilaya ya Musoma Mjini kwa nyakati tofauti wanasiasa hao walitumia jukwaa kulaani matukio ambayo yamekuwa yakitokea yakiwemo ya mauaji.

Awali Mbunge wa jimbo la Musoma Mjini Visenti Nyerere alitumia jukwaa hilo kusikitishwa na kitendo cha Mkuu wa Wilaya kushindwa kufika katika mkutano huo licha ya kualikwa kutoa ufafanuzi kwa Wananchi kutokana na matukio mbalimbali ya mauaji ambayo yamekuwa yakitangazwa na yeye kukanusha.

"Akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya tumemualika kuja kutoa ufafanuzi kwa Wananchi juu ya yale yanayoelezwa lakini ameshindwa kufika na matokeo yake anatutumia ujumbe kwa njia ya simu akisema yupo kwenye sherehe za miaka 51 ya Uhuru huu si uungwana na tunasema yeye ameshindwa kuja tukisikia mtu mwingine amekufa tutaandamana kushinikiza aondoshwe katika Wilaya hii.

"Sisi hatutaki kujua idadi ya watu waliofikwa na matukio ya kuchinjwa hata kama amechinjwa mtu mmoja suala ni kutokea kwa tukio hilo hivyo akiwa kama mkuu wa Amani katika Wilaya alipaswa kuitika wito wa Mkutano huu na kuwaondoa hofu Wananchi kutokana na yale yaliyoelezwa",alisema Nyerere

Alisema suala hilo halikuwafurahisha lakini pia Mbunge huyo akamtaka Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mara Absalom Mwakyoma kukatisha likizo yake ili kuja kutoa ushirikiano katika kukabiliana na matatizo yaliyojitokeza katika siku za hivi karibuni hali iliyopelekea Wananchi kuwa na hofu na kushindwa kufanya shughuli za kimaendeleo.

Akizungumzia suala la Maendeleo Nyerere alisema akiwa kama Mbunge kwa kushirikiana na Balaza la Madiwa linaloongozwa na Chadema watahakikisha yale yote waliyoyaleza katika kipindi cha kampeni yanatekelezwa nakuomba Wananchi waendelee kutoa ushirikiano katika kufanikisha.

"Wananchi wenyewe mnaona kwa kipindi cha muda mfupi barabara nyingi ambazo zilikuwa hazipitiki lakini leo zinapitika na kufika katika maeneo mbali yaliyokuwa korofi na haya ni maeneo machache katika miundombinu lakini pia hata katika miradi mingine ikiwemo ya maji utekelezaji wake unafanyika.

"Tumepata Bilioni 13 kutoka benki ya Dunia katika miradi ya barabara tunawahahakishia Wananchi fedha hizi zitafanya kazi kama zilivyoelekeza na zipo barabara ambazo zitakuwa na kiwango cha lami na nyingine za kiwango cha changarawe na tunataka kufikia mwaka 2013 mwishoni kila barabara iweze kupitika.

Kwa upande wake aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Godbles Lema yeye aliwataka Wananchi kutokuwa moyo wa uoga katika kudai haki zao za msingi na kutoa ushirikiano na kushirikiana na viongozi wa Chadema katika kutafuta mabadiliko na badala yake kukaa pembeni na kuanza kulalamikia kila wakati.

"Nimewapenda vijana wa Musoma nyie ni Jasiri kama walivyo vijana wa Arusha ambao kila kukicha wanatamani mabadiliko lakini naamini ipo siku itafika na kile tunachokitaka kitafanikiwa lakini nawaomba ondoeni moyo wa uoga jengeni ujasiri na shirikianeni na viongozi wenu katika kutaka kujikomboa.

"Haina maana kila wakati kukaa pembeni na kuanza kulalamika maana mabadiliko hayaji kwa kulalamika tujitoe na tushirikiane katika kufanikisha kile ambacho tumekuwa tukikitaka ili kila mmoja aweze kunufaika na rasilimali zilizopo katika Nchi hii ambazo zimekuwa zikiwanufaisha watu wachache",alisema Lema

Lema alisema kila mmoja kwa nafasi yake anao wajibu wa kuhakikisha analeta mabadiliko na sio kazi ya kuwaachia viongozi pekee yao katika kuyatafuta huku wengine wakikaa pembeni na kuanza kulalamika kwani malalamiko yao yatakuwa hayana maana katika kufikia malengo ambayo yanakusudiwa.

Friday, December 7, 2012

MARA PRESS CLUB TARIME

waandishi wa habari wakipiga picha na dc wa tarime mh hejewele ni katika semina ya ukatili wa jinsia kwa kinamama na watoto wa kike



TAALIFA YA JESHI LA POLISI MARA

JAPHET LUSINGU-KAIMU KAMANDA WA POLISI MARA, MUSOMA

Jeshi la Polisi Mkoani Mara limekanusha uvumi wa kutishia wananchi toka kwa baadhi ya watu wenye nia mbaya kuwa ndani ya mwezi mmoja watu 15 wameuwawa kwa kuchinjwa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kaimu kamanda wa Jeshi la Polisi Mara, Musoma Japhet Lusingu imedai kwamba hivi karibuni kumekua na uvumi kuwa katika Mkoa wa Mara wananchi wamekuwa wakichinjwa na tayari watu 15 wameuwawa kwa kuchinjwa kitu ambacho ni uongo.
Kaimu kamanda huyo amesema kutokana na uvumi huo wamekua wakipokea simu toka kwa wananchi na viongozi ndani ya manspaa ya Musoma katika kata ya nyakato kwamba kuna kuna mwanafunzi ameonekana ameuwawa kwa kukatwa kichwa katika makaburi ya Musoma bus na jeshi la polisi likifuatilia wanakuta ni taarifa za uongo na za kuwatisha wananchi.
Amesema kuna matukio mawili wanawake kuuwawa vichakani katika vijiji vya Mmahare kata ya Etaro ambapo Blandina Peru (28) aliuwawa 2.12.2012 kwa kukatwa koromeo na kubakwa na wauaji kabla ya kumuua wakati akiwa porini akikata kuni na watuhumiwa wa tukio hilo bado hawajakamatwa.
Tukio la pili lilitokea Kabegi kata ya Nyakatende wilayani butiama ambapo Sabina Mkireri (44) mkazi wa kijiji cha kiemba aliwawa kwa kuchinjwa shingo na kichwa chake kuchukuliwa na watu wasiojulikana katika kijiji cha kabegi na watu sita wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano.
Kutokana na uvumi huo amewatoa hofu wananchi  juu ya mauaji hayo na kuwatahadharisha akina mama hasa maeneo ya vijijini wanapokua katika shughuli zao za kilimo na utafutaji wa kuni wawe waangalifu na watoe taarifa mapema wanaposhuku jambo lolote lisilo lakawaida.
Ameongeza kuwa kwa sasa wanaendelea na msako maeneo mbalimbali ya manispaa ya Musoma na wilaya ya butiama ambapo kuna watu watano wanashikiliwa na jeshi hilo kwa kwa makosa yakupatikana na pombe haramu ya gongo na wengine wanashikiliwa kwa kupatikana na bangi na wote watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
Katika hatua nyingine amewataka wananchi wenye taarifa za uhalifu na wahalifu wasisite kulijulisha jeshi la polisi kupitia kwa viongozi wa maeneo yao.